Popular Posts

Monday, 20 May 2013

USHAURI WA MH. MSIGWA ULISINGEPUUZWA VURUGU ZA IRINGA ZISINGETOKEA



Wiki iliyopita Mh. Peter Msigwa aliongelea tatizo la Wamachinga wa Iringa.



Alishauri yafuatayo:



1. Serikali ifanye mpango wa kuongea na wamachinga na kupata suluhisho la pamoja. Anasema kuwa Mwanza, Mbeya na Moshi wakuu wa Mikoa walikuwa tayari kuongea na wamachinga wa huko na tatizo lao likatatatuliwa.

2. Alionya juu ya kutumia nguvu za polisi kama suluhisho la suala hili, kwa kuwa hawa ni wananchi wenye shida inayohitaji kutatuliwa, hivyo ni busara wasikilizwe kuliko kutishwa na kuletewa polisi.

3. Alionya kuwa Polisi wanapotumika kuzuia sauti za wamachinga, wanatengeneza mazingira ya wananchi kuchukia serikali yao na kuona inawakandamiza.

Angalia zaidi video hii, BOFYA HAPA CHINI



MCHANGO WA MH. PETER MSIGWA BUNGENI

No comments:

Post a Comment