Wiki
iliyopita Mh. Peter Msigwa aliongelea tatizo la Wamachinga wa Iringa.
Alishauri
yafuatayo:
1.
Serikali ifanye mpango wa kuongea na wamachinga na kupata suluhisho la pamoja.
Anasema kuwa Mwanza, Mbeya na Moshi wakuu wa Mikoa walikuwa tayari kuongea na
wamachinga wa huko na tatizo lao likatatatuliwa.
2.
Alionya juu ya kutumia nguvu za polisi kama suluhisho la suala hili, kwa kuwa
hawa ni wananchi wenye shida inayohitaji kutatuliwa, hivyo ni busara
wasikilizwe kuliko kutishwa na kuletewa polisi.
3.
Alionya kuwa Polisi wanapotumika kuzuia sauti za wamachinga, wanatengeneza
mazingira ya wananchi kuchukia serikali yao na kuona inawakandamiza.
Angalia
zaidi video hii, BOFYA HAPA CHINI
MCHANGO WA MH. PETER MSIGWA BUNGENI
No comments:
Post a Comment